Monday, November 5, 2018

Chalinze Eneo Ghafi Tanzania


Halmashauri ya Chalinze kwa Mkoa wa Pwani ni halmashauri ghafi kwa maana kwamba ni kiini cha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini inayotekelezwa kwa kasi.ninaposema ni halmashauri ghafi au eneo ghafi ni eneo lenye madini mbalimbali ya ujenzi kama mchanga,mawe,kokoto na mawe mbalimbali yanayotumika kutengeneza vigae katika viwanda vyetu hapa nchini.
Kwa upande wa kokoto inayopatikana Chalinze ni kokoto bora katika Afrika Mashariki inayotumika katika ujenzi wa reli ya kisasa yaani “Standard Gauge Railway”kokoto hii ni kokoto inayokubalika kimataifa ni kokoto ambayo inatumika katika ujenzi wa reli hii ambayo ni mradi wa kitaifa ambao kimsingi serikali ya awamu ya tano inautekeleza kwa kasi ya hali ya juu,hivyo utekelezaji wa mradi huu hatuwezi kusema tunatekeleza pasipo kuitaja Chalinze.
Aidha tuna mradi mwingine ambao umekwisha kamilika katika jiji la Dar es salaam,mradi wa daraja la juu yaani “Flyover”mradi huu umejengwa kwa kutumia kokoto inayotoka Chalinze kuanzia mwanzo wa ujenzi hadi mwisho,kwa hiyo bado wanachalinze na Pwani kwa ujumla tutaendelea kujivunia Chalinze kama eneo ghafi lenye fursa za kutosha katika kukuza uchumi wa Tanzania kupitia matumizi sahihi ya mali ghafi inayopatikana Chalinze.



 

 

 

 

Kokoto ya Chalinze ni kokoto bora inayotumika katika ujenzi wa miradi mbalimbali ya serikali na ya ile sekta binafsi kwa maana ya ujenzi wa nyumba binafsi,majengo ya umma,barabara na madaraja mbalimbali katika kuboresha miundombinu ya barabara nchini.
Serikali iko katika maandalizi ya ujenzi wa mradi mkubwa wa kufua umeme wa maji katika bonde la mto Rufiji,mradi ambao utaondoa kero ya upungufu wa umeme nchini.Katika ujenzi wa mradi huu kokoto itakayotumika ni kokoto kutoka Chalinze,kiasi kikubwa cha kokoto kitatumika katika utekelezaji wa mradi huu.
Hivyo dhana ya Chalinze kuwa Eneo Ghafi la utekelezaji wa ujenzi wa miradi mbalimbali ya kitaifa itaendelea kuishi siku zote na tutaendelea kusema” Chalinze Eneo Ghafi,Chalinze kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Ujenzi kitaifa”