Wednesday, May 2, 2018

Zingatieni Sheria na maadili ya kazi-RC Pwani


Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo awataka waajiri na wafanyakazi kuheshimu sheria za utumishi wa umma kwa kila mmoja kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria za nchi,ameyasema hayo katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani yaliyoadhimishwa kimkoa katika halmashauri ya Mji wa Kibaha Jana katika viwanja vya shirika la elimu Kibaha na kukemea tabia za baadhi ya waajiri wasiotaka kufuata sheria za utumishi kwa kunyanyasa wafanyakazi hatakuwa tayari kufanya kazi na watu wa aina hiyo katika mkoa wa Pwani.


Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo(katikati) akiimba wimbo wa wafanyakazi

Wafanyakazi bora wa halmashauri ya wilaya ya Chalinze katika maandamano

Wafanyakazi hodari kutoka halmashauri ya Chalinze wakiwa na furaha kwa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani

Wafanyakazi bora wakiongozwa na afisa utumishi wa Chalinze Ruth Timba

Wafanyakazi hodari wakiwa katika viwanja vya shirika la elimu kibaha

Chalinze Hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

Hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

Hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

Meza kuu wakati wa Mei Mosi 2018

Viongozi mbalimbali katika maadhimisho ya mei mosi 2018

VIongozi mbaimbali

Wafanyakazi hodari baada ya kutunukiwa zawadi zao

Solidarity forever

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chalinze,Bwana Edes Lukoa Akijitambulisha katika kusanyiko la mei mosi

Wafanyakazi hodari wakipeana hongera

Mkuu wa Mkoa wa Pwani akitoa hotuba yake katika siku ya Mei Mosi

Wafanyakazi wa Chalinze ktika picha ya pamoja na Mkurugenzi wao

Picha ya Pamoja baada ya maadhimisho

Akisoma Risala ya shirikisho la wafanyakazi(TUCTA )Mkoani Pwani Bwana Ramadhani Kinyagoli aliishukuru serikali kwa jitihada zake katika shughuli za maendeleo zinazotekelezwa na serikali ya awamu ya tano kwa maslahi ya watanzania wakiwemo na wafanyakazi,hata hivyo hakusita kuwasilisha madai na changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyakazi wa mkoa wa Pwani ikiwa ni pamoja na wafanyakazi kutopandishwa vyeo kwa wakati,kodi kubwa ya mshahara,wastaafu kutolipwa mafao yao kwa wakati,waajiri kutoheshimu sheria za utumishi kwa kutowatendea haki watumishi kwa kuwapa maslahi yao kwa mujibu wa sheria,sekta binafsi kuwazuia watumishi kujiunga na vyama vya wafanyakazi na baadhi ya halmashauri kutoitisha vikao vya mabaraza ya wafanyakazi.
Kinyangoli aliendelea kufafanua kero zinazowasibu wafanyakazi katika mkoa wa Pwani kwa kutoa shutuma kwa baadhi ya waajiri kutotimiza ahadi zao kwa wafanyakazi hodari wa mwaka jana kwa kutowapa zawadi zao hadi sasa na kuomba Uongozi wa mkoa ulifanyie kazi kwa waajiri hao kwani ahadi zisizotekelezeka kwa wakati huvunja moyo wa utendaji kazi kwa wafanyakazi wa sekta binafsi na serikali.
Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo,katika hotuba yake baada ya risala ya wafanyakazi wa mkoa wa Pwani aliwapongeza wafanyakazi hodari kwa mwaka 2018 kwa utendaji mzuri hata wakaweza kuteuliwa kuwa watumishi hodari kutoka katika taasisi zao.Aliendelea kulipongeza shirikisho la wafanyakazi mkoa wa Pwani kwa risala nzuri iliyosheheni mambo mazuri na yenye tija kwa mstakabari wa utumishi nchini na kusema hakika risala hii imejaa “Nondo za kutosha”Ndikilo alisema.
Mheshimiwa Ndikilo katika hotuba yake aliahidi kuzifanyia kazi changamoto zinazo wakabili wafanyakazi ambazo ziko ndani ya uwezo wake na kwa zile zilizo nje ya uwezo wake aliahidi kuziwasilisha kunakohusika kwa hatua zaidi. Aliwataka watumishi wa serikali na sekta binafsi kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni katika utumishi sanjari na maadili ya kazi kwa mujibu wa taaluma walizonazo.Aliwataka wafanyakazi kujiepusha na matendo ya utovu wa nidhamu katika kazi.”Lazima tuwe na nidhamu ya kazi uvivu kazini ni sumu katika ajira”Ndikilo alisema.
Aidha Ndikilo alisikitishwa na kitendo cha waajiri wanaotoa ahadi hewa kwa watumishi hodari na kutowatunuku zawadi zao kwa wakati hili halikubaliki hata kidogo na kutoa onyo kwa waajiri wanaobagua wananchi katika ajira hususan watu wenye ulemavu na wanawake na alisisitiza sitakuwa tayari kufanya kazi na wawekezaji wa aina hii kwani wanafanya vitu vilivyo kinyume na katiba na sheria za nchi pia.
Mwisho Mkuu wa mkoa aliwataka waajiri kuacha tabia ya kuzuia watumishi kuhama kutoka kituo kimoja kwenda kituo kingine ni haki ya mtumishi hivyo kukubali au kukataa uhamisho ni jukumu la wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa si suala la mwajiri.”Kama mwajiri toa maoni yako katika barua ya mtumishi na siyo kumzuia au kukataa kumpitishia barua yake ni kosa mruhusu na TAMISEMI wataamua”.Ndikilo alisema.