Tuesday, July 18, 2017

Tangazo la kazi

HALMASHAURI YA WILAYA YA KISHAPU

TANGAZO LA KAZI ZA MKATABA


Mkurugenzi mtendaji Wilaya ya Kishapu anawatangazia wananchi Raia wa Tanzania wenye sifa ya kuomba nafasi za kazi za mkataba kama ifuatavyo:-
1.     Msaidizi wa Hesabu ( Accounts Assistant ) – Nafasi 4
i.                   Sifa za Mwombaji
-         Elimu ya Kidato cha nne
-         Wenye cheti cha ATEC level II au “Foundation Level” kinachotolewa na NBAA.
ii.                 Majukumu/Kazi atakazokuwa anafanya
-         Kuandika na kutunza “Register” zinazohusu shughuli za uhasibu.
-         Kuandika hati za malipo na hati za mapokezi ya fedha.
-         Kutunza majalada ya Kumbukumbu ya hesabu.
-         Kupeleka nyaraka/barua za Uhasibu Bank.
-         kufanya usuluhisho wa masurufu, karadha, hesabu za banki na Amana.
iii.              Ngazi  ya Mshahara
-         mwombaji atayaebahatika kuajiriwa kwa mkataba ataanza na Mkataba wa malipo ya Tshs. 390,000 kwa mwezi ngazi ya TGS B
iv.              Masharti ya jumla ya muombaji kazi ya Mkataba.
-         Awe Raia wa Tanzania.
-         Awe na miaka 18-45.
-         Awe hajawahi kufukuzwa kazi, kupunguzwa, kuachishwa au kustaafishwa kazi katika Utumishi wa Umma.
-         Awe tayari kufanya kazi kituo chochote cha Afya ndani ya Wilaya ya Kishapu.
-         Mkataba utakuwa ni wa mwaka mmoja mmoja kwa kipindi chote cha mfadhili na Mkataba utarudiwa kulingana na utendaji kazi na maadili ya mtumishi.
-         Kipindi cha mfadhili kikikoma mtumishi hataingizwa moja kwa moja kwenye Ajira za Serikali.
-         Waombaji waambatishe vivuli vya vyeti vya Shule, Taaluma, Kuzaliwa na vitambulisho vya Taifa kwa wale walioandikishwa.
-         Kila mwombaji aambatishe na picha ndogo 2 passport size zilizopigwa hivi karibuni.
-         Siku ya usaili kila mwombaji afike na vyeti halisi vya shule, Taaluma, kuzaliwa na kitambulisho.
-         Kila mwombaji aandike kwa ushihi anwani yake na namba ya simu inayopatikana muda wote kwa ajili ya mawasiliano.
-         Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 27/07/2017
-         Maombi yote yaandikwe kwa mkono bila kuchapwa.
-         Maombi yote yawasilishwe kwa anwani ifuatayo:-
                       
                        Mkurugenzi Mtendaji (W)
                        S.L.P 1288
                        KISHAPU

NB:
Masharti yaliyoainishwa kwenye Tangazo hili yasomwe kwa makini na yazingatiwe



Stephen M. Magoiga
Mkurugenzi Mtendaji (W)
KISHAPU

Nakala:
1.     Katibu Tawala (M) – Kwa taarifa
2.     Mkuu wa Wilaya
3.     Waheshimiwa Madiwani – Watangazieni wananchi
4.     Watendaji Kata Wote – Tangazeni mbao za Matangazo
5.     Mbao za Matangazo zote Halmashauri ya Wilaya Kishapu.